Psalms 32:1-5

Furaha Ya Msamaha

Zaburi ya Daudi. Funzo.

1 aHeri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake,
ambaye dhambi zake zimefunikwa.
2 bHeri mtu yule ambaye Bwana
hamhesabii dhambi,
na ambaye rohoni mwake
hamna udanganyifu.

3 cNiliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa
kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
4 dUsiku na mchana
mkono wako ulinilemea,
nguvu zangu zilinyonywa
kama vile katika joto la kiangazi.
5 eKisha nilikujulisha dhambi yangu
wala sikuficha uovu wangu.
Nilisema, “Nitaungama
makosa yangu kwa Bwana.”
Ndipo uliponisamehe
hatia ya dhambi yangu.
Copyright information for SwhNEN